Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Wizara ya Katiba na Sheria

Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo Tanzania (LST)

lst Logo
UJUMBE KUTOKA KAMISHENI YA UMOJA WA AFRIKA WATEMBELEA LST
06 Jun, 2026
UJUMBE KUTOKA KAMISHENI YA UMOJA WA AFRIKA WATEMBELEA LST

Ujumbe kutoka Kamisheni ya Umoja wa Afrika (Africa Union Commission) ulitembelea Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo Tanzania (LST) tarehe 22 Mei, 2026 jijini Dar es Salaam.

Ujumbe huo uliongozwa na Mshauri wa Sheria na Kaimu Mkurugenzi wa Itifaki wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika, Prof. Hajer Gueldich ambaye aliongozana na Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Dunia ya Haki, Mhe. Abdulqawi A. Yusuf, Afisa Mkuu wa Sheria wa Umoja huo Bi. Mtendere Gondwe pamoja na Afisa Sheria Mshiriki wa Umoja huo, Bw. Stephen Buabeng-Baidoo.

Ujumbe huo uliongea na Menejimenti kuhusu dhumuni la ziara yake na majukumu yanayotekelezwa na Taasisi. Pia ujumbe huo ulipata fursa ya kuongea na wanafunzi wa kundi la 42 kuhusu mfumo wa utoaji haki wa Umoja wa Afrika.

Online Help
Kuanzisha Enzi Mpya katika Udhibiti wa Sekta ya Michezo ya Kubahatisha nchini Tanzania
https://saris.lst.ac.tz/Registrations

" >